ndugu yangu kuna suali muhimu sana kwa kila moja wetu ajiulize je! baada yakifo waenda wapi.? hili ni suala yatakika kila muislamu aliweke akili mwake,kwa sababu siku ya kiyama hakuna sehemu ya mtu atakapo enda ima ni peponi ama ni motoni kwa hivyo nitufanye amali njema zitakazo tufaa siku ya kiyama.
Kuunga vizazi ni jambo ambalo kwalo Mwenyezi Mungu Anakunjua riziki, Anarefusha umri na Anabarikia mali ya mtu. Kuunga vizazi ni alama ya ukamilifu wa Dini na uzuri wa Uislamu. Na kukata kizazi ni sababu ya kulaaniwa na kuteswa, kupata maangamivu na adhabu, kinafuta baraka na kinarithisha uadui na machukivu.
Kuamiliana na nyoyo ili kuzivuta ni ujuzi unaohitaji mtu auelewe vizuri. Na mtu anayetaka kufaulu katika kuamiliana na nyoyo hana budi ajue funguo na lugha ya nyoyo, na awe na yakini kuwa kila moyo una ufunguo wake ambao bila ya ufunguo huo hataweza kuingia kwenye moyo huo. Miongoni mwa hizo ni kutabasamu, kunza kupiga salamu, kupa tunu na mfano wa hayo.
uislamu ni dini inao amrisha watu kuhurumiana na kusikitikiana,na muislamu bora ni yule ambae atakuwa na ruhuma na ndugu zake waislamu.na mtume s.a.w ametuhimiza hilo akisema wahurumeni walio ardhini na atawahurumia alie mbinguni,na sifa ya rehma ni katika sifa za mwenyezi mungu alie tukuka,na mbwana mtume muhammad s.a.w alikuwa nimwingi wasikitiko na ruhuma kwa umma wake wote
Send your mail to recive the latest update our work in your mail your mail to recive the latest ypdates